MAJERAHA YA FIMBO KAMA YANAVYOONEKANA Dada Mesoni Kashiro (15) mkazi wa kijiji cha Gelailumbwa kata ya Gelailumbwa wilaya Longido Mkoani Arusha, ameshambuliwa na mume wake Namendea Lesiria kwa kushirikiana na rafiki yake ambaye jina halijafahamika kwa kosa la kumwaga dawa ya mfugo aina ya mbuzi.
Unaambiwa walimfunga kwenye mti wakaanza kumcharaza viboko.
Taasisi za kuzuia ukatili wa ndoa za utotoni na mateso ya utumwa zimeombwa kufuatilia hili jambo na haki itendeke kwa mtoto huyu kwanza kwa kuolewa akiwa mdogo pili kukosa haki yake ya malezi na makuzi kama mtoto na tatu kwa kupigwa kipigo kikali kisicholingana na umri wake
1 Maoni
Tatizo la uwepo wa haki za binadamu kwa upande mwingine ni kikwazo cha Utekelezaji wa sheria ya mtoto na 21 ya mwaka 2009 na marekebisho yake. Kwasababu huyu aliyetenda makosa haya, yeye mwisho wa siku atafungwa miaka kadhaa tu na kutoka huku akiwa hana makovu yoyote mwilini mwake ambayo yanaweza kuwa yanamkumbusha ukatili aliomfanyia mkewe. Pendekezo, sheria ifanyiwe marekebisho, mtu akifanya ukatili wa jinsi hii, acharazwe kwanza bakora zenye kumtia alama za kudumu kama alivyomfanyia mwenziye, ndipo sasa ahukumiwe kwenda jela. Na Nchi yetu ipunguze kuridhia ma mikataba kama haya bila kuangalia siku za usoni itskuwaje
JibuFuta