LEONARD BUGOMOLA

MSTAHIKI MEYA MANISPAA YA GEITA

Baraza la Madiwani la Manispaa ya Geita limepitisha kwa kauli moja azimio la kusitisha mkataba wa uwajibikaji kwa jamii (CSR) kati ya Manispaa hiyo na Mgodi wa GGML katika miradi miwili  ukiwemo ujenzi wa uwanja wa mpira wa Magogo.


Na kwanza tamko rasmi la kusitisha mkataba baina ya GGML na Halmashauri  likasomwa na Naibu  Meya wa Manispaa ya  Geita Elias Ngole……

Uamuzi huo umehusisha miradi mikubwa miwili iliyokuwa ikitekelezwa kwa ushirikiano na mgodi huo, ambayo ni ujenzi wa soko la dhahabu pamoja na uwanja wa mpira wa Magogo.

ENG CHACHA WAMBURA

MBUNGE WA JIMBO LA GEITA MJINI

Madiwani wameeleza kusikitishwa na kuchelewa kwa utekelezaji wa miradi hiyo, hali ambayo imewafanya kufikia uamuzi wa kusitisha mkataba huo.

Katika sakata hilo, suala la ujenzi wa Uwanja  mpira wa Magogo limeonekana kuwa miongoni mwa ajenda muhimu, kutokana na wapenzi wa soka kuendelea kuhoji maendeleo ya ujenzi  huo.

ELIAS NGOLE

NAIBU MEYA MANISPAA YA GEITA

Meya wa Manispaa ya Geita Leonard Bugomola amesema kama Manispaa hawataki fedha bali walitaka kuona matokeo chanya kwenye mradi wa uwanja.


Na hapa Mkurugenzi wa Manispaa ya Geita Yefred Myenzi anapokea azimio hilo kwa autekelezaji.