*MWANANCHI WA KIJIJII CHA BWANGA WAKIMSIKILIZA KATIBU WA NEC ITIKADI, UENEZI NA MATUNZO PAUL MAKONDA ALIPOKUA KATIKA ZIARA YAKE MKOANI GEITA*

 

MAKONDA AWATAKA WANANCHI KUWA WALINZI WA AMANI.


N.A. ROSE MWEKO, GEITA. 


KATIBU wa NEC Itikadi, uenezi na mafunzo Paul Makonda amewataka wananchi wa mji wa katoro/Buseresere kuwa walinzi wa amani kwa kuhakikisha wanawabaini na kuwafichua waharifu  na watu wanaofanya ukatili wa binadamu katika mji wa katoro na maeneo yote ya kanda ya ziwa ili kuifanya kanda hii kuwa sehem salama ya kuishi.



Makonda alisema mji wa katoro na Buseresere ni mji wa kibiashara unapaswa kuwa na amani na utulivu ili kuwafanya wananchi kufanya kazi za kujitafutia riziki wafanye kwa amani na utulivu ambapo kwa kufanya hivyo Serikali itajiongezea kipato kwa kukusanya kodi.


" ndugu zangu niwaombe kila mtu awe mlinzi wa mwenzie kwa kusimamia ulinzi ikiwemo ni ulinzi dhidi ya waharifu pia ulinzi ulinzi dhidi ya watu wenye kutenda uharifu kwa watoto, wanawake na jamii kwa ujumla kwani vitendo hivi vinadumaza maendeleo ya Taifa" alisema Makonda.





Alipotaka kujua utekelezaji wa  mradi wa maji  Katoro /buseresere Makonda alimpigia simu Waziri wa Maji Juma Aweso ambapo alisema  mradi  huo maji umegharimu zaidi ya billion 6 .5 ambapo mpaka sasa ujenzi umeshakamilika kwa aslimia 92  na inatarajiwa kukamilika asilimia 100 ndani ya wiki tatu kutoka sasa .



Aweso alisema kuna mradi mkubwa wa maji utakaonufaisha miji zaidi 28 ikiwemo mikoa ya Kanda ya ziwa na inatarajiwa kuwa mpaka kufikia 2025  mradi huo utakua umekamilika kwa zaidi ya asilimia 95 ya upatikanaji wa maji safi na salama.



" Geita ina vijiji 486  ambapo mpaka  zaidi ya 333  vimeshapatiwa maji na tayari zaodi ya billioni 24  zimeshatolewa ili kutatua changamoto ya maji  ambapo tayari Serikali imeshanumua Mitambo 25 ikiwa kila Mkoa ulipatiwa mtambo 1 utakaowawezesha kuchimba kisima katika maeneo ambayo hayatafikiwa na maji mkubwa" alisema Aweso.



" Tanzania ina Vijiji 12318  ambapo tayari vijiji 9675  vimeshapatiwa maji  na vijiji 1500 miradi inatekelezwa " alisema Aweso


Katika utekelezaji wa ilani ya uchaguzi katika Barabara 

 Makonda alimtaka meneja wa TARURA Wilaya ya Geita mhandisi Bahati  Subeya kutoa ufafanuzi wa ujenzi wa barabara za mitaani kwa kiwango cha lami


Katika mji wa katoro/ Buseresere Tarura ina kilomita 153 ambapo mpaka sasa Tayari kilomita 2 za lami  katoka mji wa Katoro  zimeshajengwa kwa gharama ya million 647.


Makonda alisema Serikali kupitia Halmashauri ya wilaya ya Geita  kuongeza bajeti yake TARURA ili kuwezesha kukidhi mahitaji  ya utekelezaji  wa miradi.


MWISHO