MAKONDA Alipotaka kujua utekelezaji wa  mradi wa maji  Katoro /buseresere Makonda alimpigia simu Waziri wa Maji Juma Aweso ambapo alisema  mradi  huo maji umegharimu zaidi ya billion 6 .5 ambapo mpaka sasa ujenzi umeshakamilika kwa aslimia 92  na inatarajiwa kukamilika asilimia 100 ndani ya wiki tatu kutoka sasa .



Aweso alisema kuna mradi mkubwa wa maji utakaonufaisha miji zaidi 28 ikiwemo mikoa ya Kanda ya ziwa na inatarajiwa kuwa mpaka kufikia 2025  mradi huo utakua umekamilika kwa zaidi ya asilimia 95 ya upatikanaji wa maji safi na salama.



" Geita ina vijiji 486  ambapo mpaka  zaidi ya 333  vimeshapatiwa maji na tayari zaodi ya billioni 24  zimeshatolewa ili kutatua changamoto ya maji  ambapo tayari Serikali imeshanumua Mitambo 25 ikiwa kila Mkoa ulipatiwa mtambo 1 utakaowawezesha kuchimba kisima katika maeneo ambayo hayatafikiwa na maji mkubwa" alisema Aweso.

" Tanzania ina Vijiji 12318  ambapo tayari vijiji 9675  vimeshapatiwa maji  na vijiji 1500 miradi inatekelezwa " alisema Aweso


Katika utekelezaji wa ilani ya uchaguzi katika Barabara 
 Makonda alimtaka meneja wa TARURA Wilaya ya Geita mhandisi Bahati  Subeya kutoa ufafanuzi wa ujenzi wa barabara za mitaani kwa kiwango cha lami

Katika mji wa katoro/ Buseresere Tarura ina kilomita 153 ambapo mpaka sasa Tayari kilomita 2 za lami  katoka mji wa Katoro  zimeshajengwa kwa gharama ya million 647.

Makonda alisema Serikali kupitia Halmashauri ya wilaya ya Geita  kuongeza bajeti yake TARURA ili kuwezesha kukidhi mahitaji  ya utekelezaji  wa miradi.

MWISHO