NA ROSE MWEKO, KAHAMA.

NAIBU WAZIRI STEPHEN BYABATO AKIKATA UTEPE KUZINDUA   UWASHWAJI  WA UMEME KWA MARA YA KWANZA KATIKA KIJIJI CHA BUTONDOLO JIMBO LA MSALALA WILAYANI KAHAMA MKOANI SHINYANGA.

ZAIDI ya Trillioni sita 6.5 zimetengwa kwa ajili ya kupeleka umeme katika vitongoji vyote Tanzania nzima katika mwaka wa fedha wa 2023-2024  lengo likiwa kuiondoa nchi gizani na kuwafanya wananchi kuendana na kasi ya maendeleo ya sayansi na teknolojia.

Hayo ameyasema  Naibu Waziri wa Nishati Steven Byabato alipokuwa katika ziara ya kukagua na kuwasha umeme katika jimbo la Masalala Wilayani Kahama, ambapo kwa jimbo la Msalala pekee zaidi ya billion 18 zimetengwa illi kukamilisha miradi ya umeme jimboni hapo.



“ Mh Rais Dkt Samia Suluhu Hassani amesema hivi anataka kabla ya kufika 2025 kila kijiji nchini kiwe kimewashwa umeme na ndio maana amepeleka fedha nyingi katika Sekta hiyo hii itasaidia kurahisisha kazi mbalimbali na ikizingatiiwa kuwa jimbo hili ni wakulima wazuri wa  mpunga tunataka wakulima wa vijiji vya Butondolo, Jana na vinginevyo waanze kuchakata mpunga hukuhuku na kupeleka Kahama mchele hiyo itasaidia kuongeza thamani ya bidhaa zetu” alisema Byabato.

Byabato alisema awali Serikali ilikua imetenga shilingi  trillion moja na billion miambili na arobaini lakini Rais Samia aliposikia kilio cha wananchi kulingana na uchache wa miundombinu iliyopelekwa vijijini aliamua kuongeza kilomita mbili kwa kwa kila kijiji na hivyo kupelekea ongezeko la fedha  la zaidi ya billion miatatu na hivyo fedha iliyotolewa ni shilingi trillion moja na zaidi ya  billion miatano.



BAADHI YA WANANCHI WA KATA YA JANA JIMBO LA MSALALA WAKIMSIKILIZA NAIBU WAZIRI NISHATI STEPHEN BYABATO(hayupo pichani) WAKATI WA UZINDUZI WA UWASHWAJI WA UMEME KATIKA KATA TATU

 “sasa wenzetu wa REA inawaagiza kufikia december  muwe mmekamilisha miundombinu yote maana wananchi hawajali nani kaleta umeme katika maeneo yao wanachikitka ni kuona umeme na sio vinginevyo na serikali kama waumishii wao tuko tayari kutekeleza hilo hivyo watendaji na wakandarasi ninawaagiza fanyeni kazi kwa haraka lakini kwa kiwango kinachotakiwa” alisema Byabato.

Iddi kasimu mbunge wa jimbo la Msalala alisema wananchi wa jimbo la Msalala walifikia hatua wakaona kuwa wametelekezwa , hii iliwasababishia wao kukata tamaa jambo ambalo hawakumuamini mtu yeyote aliyefika jimboni hapo kuomba ridhaa ya kuwa mwakilishi wao hivyo amemuomba Naibu Waziri kuhakikisha anasimamia ahadi ya umeme kuwaka kil kijiji inatimia.



NAIBU WAZIRI STEPHEN BYABATO AKIFAFANUA JAMBO KATIKA MKUTANO JIMBO LA MSALALA.

“kama mnakumbuka tulifika Msalala kuwaomba kura na tuliahidi kuwaletea maendeleo nanyi mkatuamini mkatupa kura sasa ni wajibu wetu kutekeleza yale tuliyoyaahidi ikiwemo kuwaletea umeme, afya , elimu na maendeleo mbalimbali na ndio maana leo tuko na Naibu Waziri wa Nishati amekuja kuzindua uwashaji wa umeme katika kata zetu tatu na niwahakikishie tu kuwa huu ni mwanzo mengi mazuri mtayaona” alisema Iddi Kasimu Mbunge wa jimbo la Msalala.


ALHAJI IDDI KASIMU MBUNGE WA JIMBO LA MSALALA AKIFAFANUA JAMBO KATIKA MKUTANO WA HADHARA.


MWISHO