MKUU WA MKOA WA KAGERA HAJJAT FATMA MWASA
Mkuu
wa mkoa wa kagera Ajat Fatma Mwassa amemwagiza mkurugenzi mtendaji wa
Halmashari ya Wilaya Biharamulo Denis Mkandala ahanzishe mchakato mpya wa
ujenzi wa shule ya msingi katika kata ya Nemba kutokana na changamoto zinazoikabili
shule ya msingi Nemba kwa kuhudumia wanafunzi zaidi ya 4,900 huku ikiwa na
vyumba vya madarasa 33 tu.
Mwassa ametoa kauli hiyo katika ziara yake wakati
akihutubia wananchi wa kata ya nemba wilayani biharamulo baada ya kupata
taarifa ya kata hiyo na changamoto zinazowakabili wanafunzi ikiwemo hatari ya
magonjwa ya mlipuko, utoro shuleni na ufahulu hafifu kutokana na idadi kubwa ya
wanafunzi
Mkuu
wa Wilaya Biharamulo ACP Adivera Bulimba amesema kuwa katika kukabiliana na
changamoto hiyo kupitia mradi wa boost wilaya hiyo imepokea fedha kutoka
serikali kuu zaidi ya milioni 106 imetolewa kwa ajili ya ujenzi wa madarasa
manne na matundu matatu ya vyoo katika shule hiyo
Katika
kuendeleza elimu mkoani humo mkuu wa mkoa wa Kagera Ajat Fatuma ameanza kwa
kuchangia matofari 2000 pamoja na mkuu wa wilaya hiyo matofari 1000
yatakayosaidia ujenzi wa vyumba vitatu vipya vya madarasa
MWISHO.
0 Maoni