Mkurugenzi Halmashauri ya Muleba - ELIAS KAYANDABILA  akikabidhi kitabu cha   siku 730 za utekelezaji wa miradi mbalimbali ya serilika kwa Mtendaji wa Kata.

Mauaji,mabishano na mapigano imetajwa kuwa sababu kubwa ya kurudisha nyuma uchumi na maendeleo wilaya Muleba huku siku 730 za Rais Dkt Samia Suluhu Hassan zikitumika kama njia ya kutegua kitendawilihicho ambacho kimekuwa gumzo kwa wakazi ndani ya wilaya hiyo.



BAADHI YA WAFANYAKAZI NA WANANCHI  WAWILAYA YA MULEBA WAKIFUATILIA HAFLA YA SIKU 730

 Akizungumza wakati wa hafla ya kuadhimisha Miaka miwili ya Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan tangu aingie madarakani, Katibu tawala wa Wilaya ya Muleba Greyson Mwengu amesema serikali haipo tayari kuona vitendo hivyo vinaendelea katika wilaya ya muleba na kusema kuwa watakuwa wakali zaidi.


Katibu tawala wilaya Mleba -  GREYSON MWENGU