NA ROSE MWEKO, GEITA
DARAJA LA KIGONGO-BUSISI LIKIWA KATIKA HATUA MBALIMBALI ZA UJENZI.
(picha na Rose Mweko)
MKUU wa Mkoa wa Geita Martine Shigela amewaambia wananchi wa Geita wajiandae kuchngamkia fursa za kiuchumi kutokana na daraja la Kigongo- Busisi kukamilika ujenzi wake kwani uwepo wa daraja hilo utarahisisha safari za kwenda Mwanza na Mikoa ya jirani.
Shigela aliyasema hayo juzi katika
kikao cha 13 cha bodi ya barabara Mkoani Geita alisema daraja hilo likikamilika
litaifanya Geita kwa lango uu la biashara na nchi jirani hivyo kuwataka wananchi
kuwa katika utayari wa kuchangamkia fursa mbalimbali zitakazojitokeza ikiwemo
ujenzi wa bomba la mafuta ambapo maandalizi ya ulipaji wa fidia kwa wananchi
unaendelea.
“tunawataka mamlaka za usimamizi wa
barabara kuendelea kuwajibika na kusimamia sheria ili kuzilinda barabara zetu
hii itasaidia kuboresha huduma katika sekta hii aidha elimu ya matumizi sahihi
ya barabara iendelee kutolewa kwa wananchi ili kuepuka mkanganyiko wa matumizi
sahihi ya barabara” alisema Shigela.
0 Maoni