MKURUGENZI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA JOHN WANGA AKIKABIDHI VITANDA 20 VYA WAGONJWA KITUO CHA AFYA KATORO
Na Rose Mweko, Geita.
MKURUGENZI wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita, Paul Wanga amesema Halmashauri ya Geita imeanza kuchukua hatua madhubuti ya kuhakikisha inamaliza kero ya uhaba wa vitanda vya wagonjwa kwenye vituo vya afya.
Wanga amesema hayo jana mara baada ya kukabidhi vitanda vya wagonjwa 20 katika kituo cha afya cha Katoro ambacho kilichokuwa na uhaba wa uhaba wa vitanda, jambo ambalo litasaidia kupunguza changamoto hiyo.
Alisema mpango huo unalenga kuwezesha vituo vya afya kumudu idadi kubwa ya wagonjwa hasa kina mama na wanaofika kupata huduma ambapo mpaka sasa kituo cha afya Katoro kinahudumia kina mama wazazi kati ya 30 hadi 40 kwa siku.
“Hii ni sehemu tu ya vitanda ambavyo tumeagiza, jumla tumeagiza vitanda 50, kwa hiyo tumeanza na 20 hivi ambavyo ndio vimefika tumevipokea, na kwa hiyo tunavileta hapa kituoni kwa ajili ya kuvikabidhi sasa.
“Sisi kama Halmashauri
ya Wilaya ya Geita tunaendelea kukamilisha hospitali yenye hadhi ya wilaya
iliyopo Katoro (mji mdogo), ianze kufanya kazi, ambapo tunatarajia kati ya
mwezi Januari 2023 hospitali hiyo ianze kutoa
huduma.
Mganga Mkuu wa
Halmashauri ya Wilaya ya Geita, Dk Modest Burchard alibainisha vitanda 20 vya
wagonjwa vimegharimu Sh milioni 14 ambapo vimeongeza idadi katika kituo cha
afya Katoro kutoka vitanda 66 hadi vitanda 86.
“Kituo chetu cha afya
kimekuwa kikipata wazazi kwa mwezi wanaojifungua takribani 900 mpaka 1000 kwa
miezi mitatu mfululizo, lakini hali hii huwa siyo ya kudumu kuna kipindi
wanajifungua 600, 700 mpaka 800.”alisema Sungura.
0 Maoni