MH ALBERT CHALAMILA MKUU WA MKOA WA KAGERA
KAGERA
Mkuu wa mkoa wa Kagera Albert John Chalamila amewataka wazazi na walezi
katika mkoa huo kuwa karibu na watoto wao ili kuwasaidia watoto hao kuwa na
malezi na makuzi bora yakatakayo leta faida kwa taifa la Tanzania.
Akizungumza katika Hafla ya Mpango Jumuishi,Makuzi,Malezi na Maendeleo ya
mtoto iliyo shilikisha Mashirika,taasisi na wadau mbalimbali Mkoani humo
amesema kuwa, mapango huo utasaidia kutengeneza mazingira mazuri yaliyosahihi
yatakayoweza kuisaidia jamii kuwa na kizazi bora bali wasipo elewa ukweli huo
itabaki katika mazingira magumu.
Katika hatua nyingine amesema kuwa unakuta mtu anamzaa mtoto leo anaenda
kumtupa wakati amelea mimba miezi tisa tumboni alafu anamtupa mtoto, amesema unakuta mzazi mmoja anataka kumkomoa
baba yake na akidai kuwa anafanya hivyo hataki mimba yake hataki mtoto, akitoa
mfano MUNGU alivyo wa ajabu mtoto anakaa hata siku tano bila kufa porini mpaka
jamii inamuokota na kumpeleka kwenye kituo cha watoto yatima.
“Kama unaona hujajiandaa kisaikirojia kuwa mzazi basi usizae na kuzaa
kusiwe na dhana katika kichwa chako kwamba umebeba mzigo wa mtu mwingine kwa
sababu ya maswala ya kupatikana kwa mtoto yana muhusisha Baba na Mama” alisema
Mh Chalamila.
Afisa Maendeo Mkoa Kagera Issa Ndimi amesema kuwa programu hiyo ilipangwa
kuanzia mwaka 2021 hadi 2025/26 na kutoa mafunzo kwa waandishi wa
habari,viongozi wa dini, na kuwasaidia kuifikishia jamii taarifa ikiwa ni lengo
la serikali pamoja na kuanzisha kona jumuishi zenye lengo la kuwahusisha watoto
na wadau mbalimbali.
Awali akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa Programu jumuishi ya
Makuzi,malezi na Maendeleo ya mtoto Katibu tawala Mkoa Kagera Toba Nguvila amesema
kuwa mpango huo ulizinduliwa na Mh. Rais kwa kuwakilishwa na Waziri Dkt. Doroth
Gwajima ambapo utasaidia katika kuhakikisha watoto wanapata malezi bora hasa
katika Mkoa wa Kagera na kama watendaji ndani ya mkoa huo wapo tayari kwa
kushirikiana na wadau mbalimbali na kuwaomba baadhi yao waanze kwa kuchangia
chakula cha mchana shuleni.
MWISHO
0 Maoni