Mkuu wa Mkoa Kagera Meja Jeneral Charles Mbuge akiongea na baraza la UVCCM Kagera

Mkuu wa Mkoa Kagera Meja Jeneral Charles Mbuge amewataka vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Mkoani humo wasitumike kama madaraja ya wanasiasa uchwala  kwa fedha ndogo ndogo za msimu bila kujali maslahi mapana ya Taifa la Tanzania.

Akizungumza kwenye kikao cha Baraza la umoja wa vijana uvccm 

Mkoani Kagera katika tathimini ya maendelo kwa kipindi cha miaka 

mitano ndani ya chama hicho Mkuu wa Mkoa amesema kuwa 

kuna baadhi ya wanasiasa wasiopenda maendeleo wamekuwa wakiwatumia baadhi ya vijana kwa masilahi yao binafsi na kushindwa kulitanguliza Taifa, wanakuwa wawanasiasa uchwala waliopitwa na wakati badala yake amewataka vijana wabadilike wawe mfano mzuri wa watangulize maslahi ya Nchi Mbele kuliko fedha za wanasiasa hao .



baadhi ya wajumbe wa umoja wa vijana wakiwa kikaoni


Awali akiwasilisha changamoto na maombi ya Baraza hilo kaimu 

mwenyekiti Bi. Sophia Busunge ameiomba serikali kuwakumbuka 

kwa kuwapatia vitendea kazi zikiwemo mashine za kufyatua 

matofari,zana za uvuvi,mizinga ya kufugia nyuki kilingana na uhitaji 

wa kila wilaya pamoja ana kuwaanzishia viwanda vidogo vidigo ili i

werahisi wao kama jumuiya kuweza kakabiliana na hali ya 

Marejesha ya mikopo na kupunza hali ya vijana kukimbia na mikopo 

kwa sasa wanahaidi kukaa katika eneo moja la kufanya kazi.


Toba Nguvila Mkuu w Wilaya ya Muleba akiongea na wajumbe wa baraza la UVCCM Mkoa wa Kagera



Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya Muleba Toba Nguvilla amewaasa vijana wa UVCC Mkoa wa Kagera wakaanzisha kambi kwa ajiri ya kufyatua tofari ili kujiandaa katika kipindi cha mvua ifanyike ujenzi tu sio kufyatua tofari ambapo amesema kuwa  viongozi wazuri ni wale wanaojitoa kwa ajiri ya kulijenga Taifa lao kwa uzalendo wataweza kumsaidia Mhe, Rais kwa maendeleo ya Tanzania na kutumia furusa hiyo kuwaeleza kuacha tabia ya kukata tamaa bali wajitolee na kuchapa kazi, tabia ya kulalamika,uvivu pamoja na utegemezi.