Picha ya Mkuu wa Wilaya Muleba Toba Nguvila.


KAGERA

Baadhi ya wafanyabiashara Nchi za jumuiya Afrika Mashariki wameiomba serikali ya Tanzania kuwaondolea vikwazo wanavyo kutana navyo katika mipaka ya nchi hiyo jambo ambalo linawapatia wakati mgumu kwenye ufanyaji wa kazi nchini.

Wakitoa kilio chao Baadhi ya Wafanyabiashara wa Nchi ya Tanzania,Burundi,Uganda na Congo katika maonyesho ya jumuiya ya Afrika Mashariki yanayoendelea Manispaa ya Bukoba Mkoani Kagera kwa Mkuu wa wilaya Muleba Toba Nguvila aliyefungua maonesho hayo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa Kagera Meja Jeneral Charles Mbuge ambapo wasema mizigo yao inashikiliwa mara kwa mara nakupelekea kukaa kwa zaidi ya siku tatu bila kufanya biashara jambo ambalo linapelekea mabalozi wa nchi hizo kwenda kuzungumza na TRA waweze kufunguliwa.



Picha ya Mratibu wa maonesho ya Afrika Mashariki Mkoani Kagera William Ruta.

Mratibu wa maonesho hayo William Ruta amesema maonesho yameanza tangu Tarehe 15 mwezi juni mwaka huu na mategemeo yao kama waandaaji yamevuka malengo ambapo washiriki kutoka mikoa  mbalimbali nchini  wamejitokeza aidha maonesho hayo yamehudhuriwa na nchi jirani za Burundi,Congo na Uganda na kutumia nafasi hiyo kuishuru serikali ya Tanzania kupitia wizara ya mambo ya nje na ushirikino wa Afrika Mashariki kwa kuwapata vibali washiriki.

kwa upande wake Mkuu wa wiliya Muleba Toba Nguvila ambaye alikuwa mgeni rasimi katika kufungua Maonesho hayo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jeneral Charles Mbuge amewata mamlaka ya mapato TRA Kuwaondolea vikwazo wafanyabiashara katika mipaka na kusema kuwa Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan amefungua mipaka yote nchini Tanzania pamoja na kuinganisha na nchi jirani ndani ya Afrika Mashariki kwa vikwazo vilivyo ongelewa hapendi vitokee Mkoani Kagera.


Picha Mbalimbali za Baadhi ya washiriki katika Maonesho ya Afrika Mashariki.