Waandishi wa habari
wanawake wacheza mechi ya kirafiki na waheshimiwa wabunge wa jamuhuri ya
muungano wa Tanzania ambapo timu ya wabunge yaibuka kidedea baada ya mheshimiwa
spika Tulia kuibuka kinara kwa kuipa timu yao magori murua
Mechi hiyo yafanyika
baada ya waandishi wahabari wanawake takribani 21 kutoka mikoa mbalimbali
Tanzania kufika Bungeni hapo wakiwa Ni wageni wa Spika.
Timu ya Bunge ya Mpira
wa Pete ya Wanawake ikiongozwa na Spika Dkt. Tulia Ackson, imeichalaza timu ya
Chama cha Waandishi wa habari Wanawake Tanzania kwa magoli 31-10 katika mchezo
wa kirafiki uliofanyika kwenye Viwanja vya Jamhuri Jijini Dodoma.
Akizungumza mara baada
ya kumalizika kwa mchezo huo Spika wa Bunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Dkt. Tulia Ackson ameipongeza timu ya Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania kwa
uthubutu wa kuweza kucheza licha ya kuonekana kutokuwa na mazoezi Huku akieleza
Siri ya mafanikio Yao .
Pia amesema Chama cha
Netball Tanzania kimepata uongozi mpya,anaamini kitakuja na mkakati mzuri wa
kuendeleza mchezo huo ili uende vizuri kama ilivyo kwa mchezo wa mpira wa miguu
hivyo wale wanaopenda kucheza waanze wakiwa wadogo na waendelee kuweka bidii
huku kwa upande wao wataendelea kutoa ushirikiano.
Wakizungumza kwa
nyakati tofauti wachezaji walikuwa na haya ya kusemaHata hivyo waandishi
wa habari Wanawake kutoka mikoa mbalimbali nchini wamefanya ziara ya siku mbili
jijini Dodoma ambapo walipata fursa ya kuhudhuria Bunge na kujifunza namna
shughuli za Bunge zinavyofanyika pamoja na kucheza mchezo huo wa kirafiki wa
mpira wa pete.
0 Maoni